Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI-KOREA KUSINI-MAREKANI

Korea Kaskazini yawarudisha nyumbani maafisa wake kutoka mpakani

Korea Kaskazini imeondoa maafisa wake katika Ofisi pamoja na jirani yake Korea Kusini, iliyofunguliwa mwaka uliopita kwa lengo la kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong UN
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong UN Photo: KCNA via KNS/AFP
Matangazo ya kibiashara

Wizara ya Ushirikiano wa nchi hizo mbili za Korea , imesema, imepata taarifa Ijumaa asubuhi kuwa maafisa wa Korea Kaskazini wataondoka baadaye Ijumaa.

Korea Kusini imesikutishwa na uamuzi huo wa Pyongyang na kutoa wito kwa maafisa hao kurejea tena haraka iwezekanavyo ili kuendeleza ushirikiano huo.

Maafisa wa juu wa Korea Kaskazini na Kusini, hawajakutana tangu kumalizika bila mwafaka kati ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un na rais wa Marekani Donald Trump waliokutana mwezi uliopita.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.