Biashara: China kutekeleza hatua ilizoafikiana na Marekani
China inatarajia kuanza kutekeleza hatua za biashara ilizoafikiana na Marekani wakati wa mkutano kati ya Marais Donald Trump na Xi Jinping, Wizara ya Biashara ya China imesema.
Imechapishwa:
"China itatekeleza mara moja makubaliano yaliyofikiwa na pande mbili kwa bidhaa za kilimo, nishati, magari na bidhaa zingine," amesema msemaji wa wizara ya biashara ya China mbele ya vyombo vya habari, Gao Feng.
Taarifa hiyo inakuja siku tano baada ya mkutano kati ya Marais Donald Trump na Xi Jinping huko Buenos Aires, hatua ambayo huenda ikapunguza vita vya biashara kati ya nchi hizi mbili zinazostawi kiuchumi duniani.
Wizara ya Mambo ya Nje ya China tayari ilitangaza siku ya Jumatano "utekelezaji wa pointi maalum ambapo makubaliano yalifikiwa" katika wa mkutano huo kando ya mkutano wa G20, lakini bila maelezo zaidi. Gao Feng pia hakueleza ni hatua gani zitakazofuata.
Tangu Beijing na Washington kutangaza kwamba wamesitisha tofauti zao katika mgogoro wao mgumu wa kibiashara.