Mlipuko mkubwa watokea nje ya Ubalozi wa Marekani Beijing
Mlipuko mkubwa umesikika Alhamisi wiki hii huko Beijing mbele ya Ubalozi wa Marekani, mashahidi meandika kwenye mitandao ya kijamii.
Imechapishwa:
Picha na video ambazo zimerushwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha moshi mkubwa ukifumba nje ya jengo la Ubalozi wa Marekani.
Hata hivyo Ubalozi wa Marekani nchini China umejizuia kusema chochote kuhusiana na hali hiyo.
Lakini chanzo cha serikali ya China kilio kuwa karibu na eneo la tukio kimethibitisha tukio hilo.
Kwa mujibu wa polisi, mlipuko huo umesababishwa na mtu ambaye amejeruhiwa akijaribu kulipua kifaa hicho.
Mtu huyo mwenye umri wa miaka 26 kutoka Mkoa wa Mongolia amelazwa hospitali, na anaendelea vizuri, polisi ya China imesema katika taarifa yake, ikiongeza kuwa hakuna mtu mwingine aliyejeruhiwa katika mlipuko.