Rais wa zamani wa Korea Kusini afikishwa mahakamani
Aliyekuwa rais wa Korea Kusini, Park Geun-Hye amefikishwa mahakamani kuanza kesi inayomkabili. Hii ni kwa mara ya kwanza aliye kuwa rais wa nchi hiyo kufikishwa mahakamni mjini Seoul kwa tuhuma za ufisadi.
Imechapishwa:
Pia ni kwa mara ya kwanza Park Geun-Hye kuonekana hadharani tangu kuondolewa mamlakani na kuzuiliwa mwezi Machi mwaka huu.
Hata hivyo Park Geun-Hye amekanusha kufanya makosa yeyote, licha ya tuhuma za ufisadi dhidi ya yake.
Bi Park alifika mahakamani akiongozana na rafiki wake wa karibu, Choi Soon-Sil ambae anatuhumiwa kwa kujipatia fedha kutoka kwa makampuni makubwa.
Park Guen-Hye aliulizwa ajira yake na kujibu hajaajiriwa.