Pata taarifa kuu

Magenge yenye silaha kero nchini Haiti

NAIROBI – Ukosefu wa usalama katika mji mkuu wa Haiti umefikia viwango sawa na nchi zilizo kwenye vita, umoja wa mataifa ulisema Jumatatu katika ripoti iliyoangazia kuongezeka kwa mauaji na utekaji nyara wa watu nchini humo.

Maofisa wa usalama nchini Haiti wanapambana kudhibiti makundi ya watu wenye silaha
Maofisa wa usalama nchini Haiti wanapambana kudhibiti makundi ya watu wenye silaha AP - Odelyn Joseph
Matangazo ya kibiashara

Magenge yenye silaha "yameedelela kushindana ili kupanua udhibiti wa eneo lao katika eneo lote la mji mkuu wa Port-au-Prince, na kuenea katika vitongoji ambavyo havijaathiriwa hapo awali," ilisema ripoti hiyo, kutoka kwa Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres.

"Pamoja na idadi kubwa ya vifo na kuongezeka kwa maeneo chini ya udhibiti wa magenge yenye silaha, ukosefu wa usalama katika mji mkuu umefikia viwango sawa na nchi zilizo katika vita vya silaha," ilieleza zaidi ripoti hiyo ya UN.

António Guterres, katibu mkuu wa UN ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuisaidia Haiti kupamabana na makundi yenye silaha
António Guterres, katibu mkuu wa UN ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuisaidia Haiti kupamabana na makundi yenye silaha AP - Paul Chiasson
Idadi ya mauaji yaliyoripotiwa nchini Haiti iliongezeka katika miezi ya hivi karibuni kwa asilimia 21, kutoka 673 katika robo ya mwisho ya 2022 hadi 815 kati ya Januari 1 na Machi 31 mwaka huu. Idadi ya utekaji nyara ulioripotiwa iliongezeka kwa asilimia 63, kutoka 391 hadi 637.

"Watu wa Haiti wanaendelea kukumbwa na mojawapo ya mizozo mibaya zaidi ya haki za binadamu katika miongo kadhaa na dharura kubwa ya kibinadamu," ripoti hiyo ilisema.

Makabiliano kati ya magenge pinzani nchini Haiti yamesababisha uharibifu mkubwa na mali ya raia
Makabiliano kati ya magenge pinzani nchini Haiti yamesababisha uharibifu mkubwa na mali ya raia © Odelyn Joseph/AP
Hali ya haki za binadamu ya watu wanaoishi katika maeneo yanayodhibitiwa na magenge "imesalia kuwa duni sana" na hali katika maeneo ambayo yanalengwa hivi karibuni na magenge "imezidi kuwa mbaya," kulingana na ripoti hiyo.

Kati ya Aprili 14 na 19, mapigano kati ya magenge hasimu yalisababisha vifo vya karibu watu 70, wakiwemo wanawake 18 na angalau watoto wawili, taarifa hiyo iliongeza.

Makundi ya yenye silaha kwa wakati fulani yameripotiwa kuwashambulia maofisa wa polisi nchini Haiti
Makundi ya yenye silaha kwa wakati fulani yameripotiwa kuwashambulia maofisa wa polisi nchini Haiti AP - Odelyn Joseph
"Ninasisitiza haja ya dharura ya kutumwa kwa kikosi maalumu cha kimataifa," Guterres alisema katika ripoti ya Jumatatu.

Guterres mwezi Oktoba alitoa mwito wa kuomba msaada kutoka kwa waziri mkuu wa Haiti Ariel Henry, akiomba baraza la usalama kutuma msaada kusaidia polisi kurejesha utulivu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.