Pata taarifa kuu
UFARANSA-MAREKANI

Macron awasili nchini Marekani, kukutana na mwenyeji wake Biden

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, amewasili nchini Marekani kukutana na mwenyeji wake Joe Biden, ambapo viongozi hao wawili watazungumzia ushirikiano na namna ya kuimarisha biashara, masuala ya usalama kati ya nchi zao, bila kusahau vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

Rais Macron akiwasili nchini Marekani, Novemba 29 2022
Rais Macron akiwasili nchini Marekani, Novemba 29 2022 AP - Manuel Balce Ceneta
Matangazo ya kibiashara

John Kirby msemaji wa Ikulu ya Marekani anayehusika na masuala ya usalama wa kitaifa, hapa anaeleza ni kwanini rais Biden ameamua kumwalika rais Macron kama kiongozi wa Kwanza wa kigeni, katika kipindi hiki cha uongozi wake.

Namna rais Biden anavyoshughulikia sera yake ya mambo ya nje, ni kuimarisha ushirikiano wake na washirika wake, kama Ufaransa ambaye ni mshirika wa muda mrefu.

Baada ya kuondoka jijini Washington DC, Macron anatarajiwa kutembelea New Orleans, êneo ambalo lina wakaazi wengi wa Ufaransa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.