Marekani: Polisi aliyehukumiwa kwa mauaji ya George Floyd akata rufaa
Polisi wa zamani wa Marekani Derek Chauvin alimeamua kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama wa kifungo ha zaidi ya miaka 20 kwa mauaji ya Mmarekani Mweusi George Floyd mwaka 2020, akitaja makosa kadhaa wakati wa kesi yake katika kesi hiyo ambayo ilionyesha mgawanyiko wa kina kwa ubaguzi wa rangi hnchini Marekani.
Imechapishwa:
Tukio hilo linamuonyesha akimbana George Floyd kwenye shigo kwa goti lake kwa karibu dakika kumi baada ya kukamatwa, alilipigwa picha na kurushwa mitandaoni na shahidi mmoja, liliozua hasira na kusababisha maandamano makubwa dhidi ya ubaguzi wa rangi na vurugu za polisi huko Marekani na ulimwenguni kote.
Hukumu ya kifungo cha miaka 22 na nusu aliyokatiwa Chauvin Juni 25 ilikaribishwa na umati wa watu nchini Haiti, ambao walihofia kuwa atafanya zaidi ya hayo ataachiliwa huru.
Chauvin ametaja makosa 14 katika kesi yake, wakati wote wa uteuzi wa majaji na kwa kuwa jaji hakuamuru kufungwa kwa faragha kwa majaji wakati wa kesi hiyo.
Pia anabaini kuwa Serikali ilikuwa ukimwonea tangu mwanzo, na anashutumu mahakama kwa "kutumia vibaya msimamo wake" kwa kukataa ombi lake la kuahirishwa kwa kesi hiyo au kuhamishiwa Jimbo lingine.