Pata taarifa kuu
MAREKANI-TRUMP-CORONA-AFYA

Madaktari: Trump anaweza kuondoka hospitalini Jumatatu

Rais wa Marekani Donald Trump bado yupo hospitalini kwa kuangalizi wa karibu baada ya kuambukizwa virusi vya Corona wiki iliyopita pamoja na mke wake.

Rais wa Marekani Donald Trump akiwapungia mkono wafuasi wake nje ya hospitlai ya kijeshi ya Walter Reed, ambapo anatibiwa baada ya kuambukizwa Covid-19, huko Bethesda, Maryland, Oktoba 4, 2020.
Rais wa Marekani Donald Trump akiwapungia mkono wafuasi wake nje ya hospitlai ya kijeshi ya Walter Reed, ambapo anatibiwa baada ya kuambukizwa Covid-19, huko Bethesda, Maryland, Oktoba 4, 2020. ALEX EDELMAN / AFP
Matangazo ya kibiashara

Wakati huu maswali mengi yakiulizwa kuhusu hali ya afya yake, Madaktari wake wanasema anaendelea vizuri na huenda akaruhusiwa kuondoka hospitalini siku ya Jumatatu, baada ya kuongezewa hewa mara mbili.

Siku ya Jumapili, rais Trump alionekana nje ya hospitali akiwa ndani ya gari akiwa amevalia barakoa, akiwapungua mkono wafuasi wake, hatua ambayo imelaaniwa na baadhi ya watu wanaosema ni hatari kwa afya za watu aliokaribiana nao.

Rais Trump ni miongoni mwa Wamarekani zaidi ya Milioni Saba ambao wameambukizwa virusi vya Corona, huku wengine zaidi ya Laki Mbili wakipoteza maisha.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.