Pata taarifa kuu
BRAZILI-CORONA-AFYA

Coronavirus: Karibu vifo 140,000 vinavyotokana na virusi vyathibitishwa nchini Brazil

Brazil imerekodi visa vipya 32,817 vilivyothibitishwa vya maambukizi ya virusi ya Corona na vifo vipya 831 vinavyotokana na janga hilo katika muda wa saa ishirini na nne zilizopita, wizara ya afya imesema hivi punde.

Brazil inaendelea kuathirika zaidi na janga la Corona.
Brazil inaendelea kuathirika zaidi na janga la Corona. REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Kufikia sasa idadi ya maambukizi nchini Brazil ni zaidi ya milioni 4.6, na karibu jumla ya vifo 140,000 vimeripotiwa, kulingana na takwimu za serikali.

Brazil ni nchi ya pili kuathirika zaidi na mgogoro wa kiafya baada ya Marekani, kwa suala la maambukizi au vifo.

Hivi karibuni shirika la Afya Duniani, WHO, lilitoa wito kwa serikali mbalimbali za dunia na viongozi wa sekta mbalimbali za kiafya kuangazia kwa umakini afya na usalama wa wahudumu wa afya na wagonjwa, hasa kipindi hiki cha janga la Corona.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, WHO liliwataka wadau husika kuchukua hatua madhubuti kuwalinda wahudumu wa afya dhidi ya dhulma na maswala mengine yanayohatarisha usalama wao.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.