Pata taarifa kuu

Kenya: Ufaransa inalenga kuimarisha uhusiano wake na mataifa ya Afrika

Nairobi – Ufaransa inasema inalenga kuimarisha uhusiano wake na mataifa ya Afrika, utakaoimarisha pande zote kwenye maeneo mbalimbali za ushirikiano wa maendeleo.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa Stéphane Séjourné na mwenzake wa Kenya Musalia Mudavadi.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa Stéphane Séjourné na mwenzake wa Kenya Musalia Mudavadi. © Musalia Mudavadi
Matangazo ya kibiashara

Kauli hii imetolewa na Waziri wa Mambo ya nje wa Ufaransa, Stephane Sejourne, jijini Nairobi, katika ziara yake ya kwanza barani Afrika kabla ya kuzuru Rwanda na baadaye Cote Dvoire.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa ameanza ziara yake barani Afrika.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa ameanza ziara yake barani Afrika. © Musalia Mudavadi

Sejourne, amesisitiza nafasi ya Ufaransa kushirikiana na mataifa ya Afrika kama Kenya kutatua changamoto za kikanda hasa mzozo wa Sudan, kuelekea Aprili 15 ambapo Ufaransa itakuwa mwenyeji wa kongamano la Kimataifa kuisaidia Sudan kupata misaada ya kibinadamu.

‘‘Lengo le kwanza ni kuwa mgogoro huo ujadiliwe na kwa hivyo lazima tuhamasishe jumuiya ya kimataifa ili ijue namna ya kufanya maandalizi pamoja na washirika wetu.’’ ameeleza Waziri Stephane Sejourne.

00:25

Stephane Sejourne- Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa

Kuhusu mpango wa Kenya kutuma polisi wake nchini Haiti, Sejourne amesema Ufaransa inaunga harakati hizo na imetoa kiasi cha yuro Milioni tatu katika mfuko wa Umoja wa mataifa ili kufadhili operesheni hiyo, ambayo Waziri wa Mambo ya nje wa Kenya Musalia Mudavadi amesema, Kenya ipo tayari kutoa uongozi.

‘‘Ufaransa kuna mambo mengi wanafahamu kuhusu Haiti na tunataka watusaidie kuelewa zaidi kuhusu oparesheni ya kimataifa ya kurejesha utulivu.’’ alisema Waziri Musalia.

00:33

Musalia Mudavadi- Waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya

Ziara ya Sejourne nchini Kenya imekuja wakati huu Ufaransa ikiimarisha uwekezaji wake kwenye nchi hiyo yenye uchumi mkubwa Afrika Mashariki, kufuatia ongezeko la kampuni za Ufaransa nchini humo kuongezeka kutoka 50 hadi 140 kwa kipindi cha miaka 10 na kuahidi kuongeza uwekezaji zaidi kwenye mapambano ya mabadiliko ya tabia nchi, miundo mbinu ya uchukuzi na michezo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.