Pata taarifa kuu

Cote Dvoire : Huduma za mtandao wa Internet imeanza kurejea

Nairobi – Huduma za mtandao wa Internet, imeanza kurejea kwenye ukanda wa Afrika ya Kati na Magharibi hasa nchini Cote Dvoire baada ya kushuhudia hitilafu wiki hii, baada ya kukatika kwa nyanya za baharini.

Nchini Cote Dvoire ni asilimia 50 ya Internet ndio iliyorejeshwa kwenye kampuni ya mawasiliano ya Orange nchini Cote Dvoire
Nchini Cote Dvoire ni asilimia 50 ya Internet ndio iliyorejeshwa kwenye kampuni ya mawasiliano ya Orange nchini Cote Dvoire © Issouf Sanogo / AFP
Matangazo ya kibiashara

Kampuni ya Internet, MainOne iliyo na ofisi zake nchini Nigeria, Ghana na Cote D’Ivoire, imethibitisha kuanza kurejea kwa huduma hiyo.

Aidha, imethibitisha  kuwa hitilafu hiyo ilisababishwa na kukatika kwa nyanya za Internet  kwenye Bahari ya Atlantic, Pwani ya eneo la Afrika Magharibi, na kukanusha madai kuwa, ilisababishwa makusudi na watu.

Hata hivyo, ripoti zinasema kuwa huduma hiyo ya Internet inarejea taratibu, lakini kwa kiasi kikubwa hali bado sio nzuri.

Nchini Cote Dvoire ni asilimia 50 ya Internet ndio iliyorejeshwa kwenye kampuni ya mawasiliano ya Orange nchini Cote Dvoire.

Mataifa sita ya Afrika Magharibi, yanayotumia laini ya simu, Djoliba, yaliathiriwa na changamoto hii, kutokana na kuunganishwa kwa mtandao huo kati ya Dakar na Abidjan.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.