Pata taarifa kuu

Muungano wa G5 Sahel kwenye njia panda ya kuvunjika

Chad na Mauritania zimeanza mchakato wa kukamilisha kujitoa kwenye muungano wa G5 ulioundwa kwa ajili ya kupambana na makundi ya kijihadi, baada ya nchi nyingine tatu ambazo zilikuwa waasisi kujitoa.

Maeneo ya mataifa ya Afrika Magharibi yanayopambana na itikadi kali
Maeneo ya mataifa ya Afrika Magharibi yanayopambana na itikadi kali AP - Francois Mori
Matangazo ya kibiashara

Muungano wa G5 Sahel, uliundwa mwaka 2014, ukijumuisha nchi za Mauritania, Chad, Burkina Faso, Mali na Niger wakisaidiwa na Ufaransa.

Baada ya siku ya Jumamosi, Burkina Faso, Mali na Niger kusema wanajiondoa kutoka kwa muungano huo, Chad na Mauritania wamefungua nafasi ya kuvunja muungano huo.

Mataifa haya yamesema yanaheshimu uamuzi wa kujitawala wa Burkina Faso, Mali na Niger.

Hili linajiri baada ya juma moja lililopita, Burkina Faso, Mali na Niger, kutangaza kuwa wana mpango wa kuunda shirikisho la pamoja kukabiliana na changamoto za usalama, wakati huu pia wakiegemea msaada kutoka Urusi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.