Pata taarifa kuu

Wakuu wa nchi za SADC wanakutana kujadili usalama wa mashariki ya DRC

Nairobi – Wakuu wa nchi za Kusini mwa Afrika SADC wanakutana kwa dharura jijini Luanda nchini Angola, kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 

Wakuu hao wa nchi za SADC waliwahi kukutana awali kujadili suala la  DRC
Wakuu hao wa nchi za SADC waliwahi kukutana awali kujadili suala la DRC © LUSA
Matangazo ya kibiashara

Mkutano huo unafuatiwa na ule uliofanyika mapema wiki hii kwa njia ya video, kuthathmini maandalizi ya kutumwa kwa kikosi  maalum cha jeshi kutoka Jumuiya ya SADC kusaidia kupambana na waasi. 

Hatua hiyo ilikubaliwa wakati wa kikao cha kwanza cha wakuu hao wa nchi, kilichofanyika mwezi Mei, lakini kumekuwa na mchakato wa miezi kadhaa kuunda kikosi hicho. 

Kuelekea mkutano huu, afisa wa serikali ya DRC amesema, kikosi cha SADC kinatarajiwa kuwasili Mashariki mwa nchi hiyo, baada ya mataifa matatu ya Afrika Kusini, Malawi na Tanzania, kuonesha utayari wa kutuma wanajeshi wao. 

Jeshi la DRC limeendelea kuimarisha vita dhidi ya makundi yenye silaha ikiwemo M23
Jeshi la DRC limeendelea kuimarisha vita dhidi ya makundi yenye silaha ikiwemo M23 AP - Joseph Kay

Serikali ya Kinshasa, ambayo imesema kikosi cha Jumuiya ya Afrika Mashariki hakijafanya vya kutosha kumaliza makundi ya waasi hasa M 23, imekuwa ikishinikiza ujio wa kikosi cha SADC kuelekea kumalizika kwa muda wa kikosi cha EAC mwezi Desemba. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.