Pata taarifa kuu

Liberia: Matokeo ya awali ya urais yanaonyesha Weah na Boakai wanakaribiana

Nairobi – Rais wa Liberia George Weah na mgombea wa upinzani Joseph Boakai wameripotiwa kuachana na nafasi ndogo zaidi katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais, huku karibu robo tatu ya kura ikiwa imepokelewa na tume ya uchaguzi.

George Weah na mgombea wa upinzani Joseph Boakai wameripotiwa kuachana na nafasi ndogo zaidi katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais
George Weah na mgombea wa upinzani Joseph Boakai wameripotiwa kuachana na nafasi ndogo zaidi katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais AFP
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa matokeo ya awali yaliotangazwa na tume ya  uchaguzi kwenye taifa hilo hapo jana Jumapili, Weah anaongoza kwa asilimia 43.8 dhidi ya asilimia 43.5 ya Boakai, akiwa na takriban asilimia 73 ya kura.

Boakai, ambaye aliibuka wa pili katika uchaguzi uliopita, alikuwa naibu wa Ellen Johnson Sirleaf alipokuwa rais
Boakai, ambaye aliibuka wa pili katika uchaguzi uliopita, alikuwa naibu wa Ellen Johnson Sirleaf alipokuwa rais AFP/File

Kufikia Jumapili, tume hiyo ilikuwa imetangaza matokeo kutoka vituo 4,295 kati ya 5,890 vya kupigia kura nchini humo.

Haya yanajiri wakati huu  ECOWAS, ikiwaonya waliokuwa wagombea wa urais nchini Liberia dhidi ya kuanza kujitangaza washindi wakati huu tume ya uchaguzi ikiendelea na hesabu ya kura, ECOWAS ikisema hilo litachangia vurugu.

Rais George Weah, anawania muhula wa pili
Rais George Weah, anawania muhula wa pili REUTERS - CARIELLE DOE

Pia imezitaka pande zote kudumisha amani wakati wakisubiri matokeo, na kuongeza kuwa watawajibishwa kwa vitendo vyovyote vinavyoweza kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani. Rais Weah anawania muhula wa pili madarakani.

Boakai, ambaye aliibuka wa pili katika uchaguzi uliopita, alikuwa naibu wa Ellen Johnson Sirleaf alipokuwa rais.

Mshindi lazima apate angalau asilimia 50 ya kura ili kuepuka duru  ya pili ya uchaguzi.

Raia wa Liberia walijitokeza kuwachagua viongozi wao wapya katika uchaguzi wa wiki iliyopita
Raia wa Liberia walijitokeza kuwachagua viongozi wao wapya katika uchaguzi wa wiki iliyopita REUTERS - CARIELLE DOE

Raia wa Liberia walipiga kura tarehe 10 Oktoba kumchagua rais, wajumbe wa baraza la wawakilishi na sehemu ya wabunge wa Seneti.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.