Pata taarifa kuu

Madagascar: Viongozi wa upinzani wazuiliwa kufanya mkutano

Nairobi – Maofisa wa usalama nchini Madagascar wamewafyatulia mabomu ya kutoa machozi viongozi wa upinzani waliokuwa wanaoongoza maandamano jijini Antananarivo, hatua inayokuja wakati huu joto la kisiasa likiendelea kupanda kuelekea uchaguzi wa urais wa mwezi ujao.

Andry Rajoelina, anawania kwa muhula wa pili
Andry Rajoelina, anawania kwa muhula wa pili AP - Gregorio Borgia
Matangazo ya kibiashara

Wagombea wa urais kumi na mmoja kati ya 13 wanaowania kiti cha urais, walikuwa wametoa wito kwa wafuasi wao kuandamana dhidi ya kile wanachodai ni kupendelewa kwa rais wa sasa Andry Rajoelina.

Raia wa nchini humo wanapiga kura kumachagua rais wao mpya tarehe 9 ya mwezi Novemba.
Raia wa nchini humo wanapiga kura kumachagua rais wao mpya tarehe 9 ya mwezi Novemba. © Laetitia Bezain/RFI

Waandamanaji hao wamesambaratishwa na maofisa wa polisi kabla ya kuwasili katika eneo walikokuwa wamekusudia kukutana.

Rais wa zamani Marc Ravalomanana ambaye pia ni mojawapo wa wanasiasa wa upinzani wanaowania katika uchaguzi huo, alikuwa miongoni mwa waandamanaji.

Rajoelina mwenye umri wa miaka 49, alijiuzulu kutoka mwezi uliopita kwa mujibu katiba ya nchi hiyo
Rajoelina mwenye umri wa miaka 49, alijiuzulu kutoka mwezi uliopita kwa mujibu katiba ya nchi hiyo © AFP/Bertrand Guay

Waandaaji wa mkutano huo hawakuwa wamepata kibali cha kufanya hivyo kutoka kwa vyombo vya usalama.

Wapiga kura nchini Madagascar, mojawapo ya mataifa maskini duniani licha ya utajiri wa rasilimali asili, wanapiga kura kumachagua rais wao mpya tarehe 9 ya mwezi Novemba.

Rajoelina mwenye umri wa miaka 49, alijiuzulu kutoka mwezi uliopita kwa mujibu katiba ya nchi hiyo akitaka kuwania tena katika uchaguzi wa mwaka huu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.