Pata taarifa kuu

Mazungumzo kuhusu ujenzi wa bwawa la Ethiopia yamerejelewa

Ethiopia imesema imeanza awamu ya pili ya mazungumzo kati yake na mataifa ya Misri na Sudan kuhusu ujenzi wa bwawa lenye utata linalojengwa na Addis Ababa katika Mto Nile, chanzo cha mzozo kati ya mataifa hayo matatu.

Misiri na Sudan zimeibua wasiwasi kuwa mradi huo mkubwa mwenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 4.2, utapunguza viwango vya maji zinazopokea kutoka mto Nile
Misiri na Sudan zimeibua wasiwasi kuwa mradi huo mkubwa mwenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 4.2, utapunguza viwango vya maji zinazopokea kutoka mto Nile Ethiopia govt
Matangazo ya kibiashara

Kupitia katika ukurasa wa X, zamani ukijulikana kama twitter, wazira ya mambo ya kigeni ya Ethiopia imethibitisha kurejelewa kwa mazungumzo hayo.

Mwezi huu Ethiopia ilitangaza kukamilisha kujaza maji katika bwawa la Grand Renaissance, hali ambayo ilikashifiwa vikali na Cairo ambayo ilisema hatua hiyo ilikuwa kinuyme cha sheria.

Mazungumzo kuhusu ujenzi wa bwawa kubwa la maji la Ethiopia yamerejelewa
Mazungumzo kuhusu ujenzi wa bwawa kubwa la maji la Ethiopia yamerejelewa © The Ministry of Foreign Affairs of #Ethiopia

Misri na Sudan zimeibua wasiwasi kuwa mradi huo mkubwa mwenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 4.2, utapunguza viwango vya maji zinazopokea kutoka mto Nile.

Mtaifa hayo mawili yamekuwa yakitaka Addis Ababa kusitisha mradi huo hadi pale ambapo makubaliano yataafikiwa kati ya wahusika wakuu kwenye mzozo huo.

Mazungumzo hayo yanalenga kumaliza mzozo kati ya nchi za Ethiopia na Misiri
Mazungumzo hayo yanalenga kumaliza mzozo kati ya nchi za Ethiopia na Misiri © The Ministry of Foreign Affairs of #Ethiopia

Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi na waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed walikubaliana mwezi Julai kutafuta suluhu katika kipindi cha miezi minne kabla ya kurejelewa kwa mazungumzo mwezi Agosti.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.