Watu 34 wamefariki katika ajali ya barabarani Algeria
Mamlaka nchini Algeria inasema takriban watu 34 wamefariki katika ajali ya barabarani katika jimbo la kusini la Tamanrasset.
Imechapishwa:
Ajali hiyo imetokea baada ya magari mawili kugongana na kuwaka moto.Watu wengine 12 wamejuruhiwa.
Eneo la Tamanrasset liko karibu na Niger na Mali.
Timu ya ulinzi wa raia imethibitisha idadi ya vifo na kusema waliojeruhiwa walipelekwa hospitalini.
Video zilizochapishwa na vyombo vya habari vya ndani, ikiwa ni pamoja na klipu iliyotumwa na Info Trafic Algerie, ilionyesha matokeo ya ajali hiyo na magari kuteketea.
Ulinzi wa raia ulishiriki picha kadhaa za ajali hiyo huku magari yote mawili yakiwa yameteketea na kuharibiwa.