Pata taarifa kuu
BENIN - SIASA- UCHAGUZI

Benin: Upinzani wapinga matokeo ya uchaguzi wa wabunge

Chama kikuu cha upinzani nchini Benin, kimekataa matokeo ya uchaguzi wa wabunge, ikidai kuwa uchaguzi huo ulikumbwa na wizi na ununuzi wa kura, ili kukipa ushindi chama cha rais Patrice Talon.

Uchaguzi wa wabunge uliofanyika nchini Benin wiki hii
Uchaguzi wa wabunge uliofanyika nchini Benin wiki hii AFP - YANICK FOLLY
Matangazo ya kibiashara

Kiongozi wa chama cha Demokrasia Eric Houndete, amesema matokeo ya uchaguzi huo, hayakubaliki baada ya Tume ya Uchaguzi kutangaza kuwa kilipata viti 28 huku chama tawala cha rais Talon, kikipata viti 81.

“Chama cha Democrat kinatupilia mbali matokeo ambayo hayakuheshimu maamuzi ya wanachi. ” amesema Eric Houndete.

Vyama vya upinzani viliruhusiwa kwa mara ya kwanza baada ya kipindi cha muda mrefu kushiri katika uchaguzi huo wa wiki hii wa wabunge.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.