BENIN- SIASA
Benin: Raia wanasubiri matokeo ya uchaguzi wa wabunge
Wananchi wa Benin, wanasubiri matokeo ya uchaguzi wa wabunge, uliofanyika jana, huku idadi ya wapiga kura ikiripotiwa kuwa ndogo.
Imechapishwa:
Cheza - 00:23
Matangazo ya kibiashara
Vyama vya upinzani, vilishiriki kwa mara ya kwanza, baada ya kususia uchaguzi wa miaka iliyopita.
Rais Patrice Talon amesema uchaguzi huo umebadilisha historia ya kisiasa nchini humo.
Daniel Quenum, ni mwangalizi wa uchaguzi huo.
“Nilitarajia kuona idadi kubwa ya watu kama ilivyokuwa mwaka wa 2019 lakini kulikuwa na taharuki jambo ambalo lilitia dosari katika demokrasia.” Amesema Daniel Quenum
Matokeo ya mwisho, yanatarajiwa kuwa wazi kwa siku chache zijazo.