Pata taarifa kuu
Kenya - Afya

EU : Yafadhili Kenya kupambana na Ebola

Ujumbe wa umoja wa Ulaya nchini Kenya, umetoa dolla 98,224.59 , kwa taifa hilo  ambapo zitatumika kuhamasisha umma dhidi ya ugonjwa wa Ebola, baada ya taifa jirani la Uganda kutangaza mkurupuko wa  ugonjwa huo Septemba 20, mwaka huu, katika wilaya ya Mubende.

Bendera ya Umoja wa Ulaya
Bendera ya Umoja wa Ulaya REUTERS - YVES HERMAN
Matangazo ya kibiashara

Mchango huo wa EU, utatolewa kupitia kwa shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya, ambapo shirika hilo litaendesha uhamasisho mbali na kutoa elimu kwa wakaazi wa Kenya, wanaoishi karibu na miji ya mipani, ya namna ya kujikinga dhidi ya Ebola.

Mradi huu wa miezi tatu unalenga zaidi ya raia 565, 000, wenyeji wa miji ya mipakani ya Busia, Bungoma, Siaya, Kisumu, Homa Bay na Migori

Elimu hii inatolewa kutokana na taasubi ambazo zimekuwepo ikiwemo kwamba Ebola inasabishwa na ushirikina, elimu hii ikilenga viongozi wa dini, waganga wa kienyeji na raia wa kawaida.

Eerikali ya Kenya, kupitia wizara yake ya afya, tayari imetoa tahadhari kwa raia wake kujikinga dhidi ya Ebola.

Serikali ya Uganda imethibitisha vifo 25 kutokana na Ebola , na wagonjwa 61 hadi kufikia Oktoba 18.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.