Nigeria - Elimu
Nigeria : Rais Buhari aagiza mawaziri kumaliza mgomo wa wahadhiri
Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari ,ameagiza mawaziri wa elimu na kazi nchini humo kumaliza mgomo wa muda mrefu wa wahadhiri.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Muungano wa wahadhiri nchini Nigeria, (ASUU), umeongoza mgomo huo tangu mwezi Februari tarehe 14 mwezi huu.
Wahadhiri hao wanagoma kushinikiza serikali kutekeleza mkataba wao wa mwaka 2009, uliolenga kuhakikisha wanapata nyongeza ya mishara mbali na miundo mbinu ya vyuo vikuu kuimarishwa, wahadhiri hao wanasisitiza mgomo huo utawafaidi zaidi wanafunzi, licha ya kuchukuwa muda wao.
Juhudi za serikali na viongozi wa wahadhiri kushiriki mazungumzo kumaliza mgomo huo hazijafua dafu.