Pata taarifa kuu
Burkina Faso - Siasa

Burkina Faso : Aliyekuwa rais Blaise  Compaore kurejea nyumbani

Aliyekua Rais wa Burkina Faso Blaise  Compaore, ambaye amekuwa uhamishoni  nchini Ivyory Coast, tangu mwaka 2014 anatarajiwa kurejea nyumbani kabla ya kumalizika kwa wiki hii.

Rais Blaise Compaore akiwa mjini Kinshasa, DRC, Oktoba 14, 2012
Rais Blaise Compaore akiwa mjini Kinshasa, DRC, Oktoba 14, 2012 REUTERS/Noor Khamis
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema  Compaore, mwenye miaka 71 anatarajiwa  kuwasili jijini Ouagadougou,  leo au siku ya  ijumaa  ili kukutana na wakuu wa jeshi katika mkutano wa marais wa zamani.

Rais huyo wa zamani aliyeongoza kwa miaka 27 kaba ya kuondolewa madarakani mwaka 2014 kufuatia maandamano ya wananchi, anarejea nyumbani kufuatia mchakato wa maridhiano ya kitaifa katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Compaore ambaye mwezi Aprili alipewa kifungo cha maisha jela kwa kuhusika na rais wa zamani Thomas Sankara, mwaka 1987, akiwa nchini Burkina Faso atapewa makaazi katika nyumba ya serikali, alikokuwa anazuiliwa  rais ambaye serikali yake ilipinduliwa na wanajeshi mapema mwaka huu, Roch Marc Christian Kaboré .

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.