Nigeria : Goodluck Jonathan kuwania urais mwakani
Aliyekuwa rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, ametangaza kuwania urais wa taifa hilo na kubadili mpango wa awali wa kutowania, Janathan akiwa miongoni mwa wanasiasa 26 ambao wametangaza nia yao ya kumrithi rais Muhammadu Buhari, ambaye kipindi chake cha kuhudumu kinakamilika mwaka ujao.
Imechapishwa:
Jonathan ambaye hivi karibuni ameonekana kuwa mwandani wa karibu wa rais Buhari, amebadili chama chake cha People’s Democratic Party (PDP), na kujiunga na kile cha rais Buhari All Progressives Congress (APC) ambacho kilimuondoa madarakani mwaka 2015.
Juma lililopita, rais Buhari aliagiza mawaziri wote wanaolenga kuwania nyadhifa za kisiasa kujiuzulu kufikia Mei 16.
Wengine ambao wametangaza kuwania urais ni pamoja na makamo rais wa sasa Yemi Osinbajo, mwenyekiti wa chama tawala Ahmed Bola Tinubu, pamoja na waliokuwa mawaziri 13 na magavana.
Wawaniaji wanaotafuta kupeperusha bendara ya chama cha upinzani cha PDP, ni pamoja na aliyekuwa makamo rais Atiku Abubakar, aliyekuwa spika wa bunge la seneti Bukola Sarak, gavana wa Sokoto, Aminu Tambuwa na gavana wa jimbo la Rivers Nysom Wike.