Pata taarifa kuu

Mafuriko yaua watu 300 Afrika kusini

Watu zaidi ya 300 wamepoteza maisha katika jimbo la la KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini kufuatia mafuriko ambayo pia yamesababisha uharibifu mkubwa wa miundo mbinu katika eneo hilo.

Nyumba zilizosombwa na mafuriko huko Ntuzuma, karibu na Durban, Afrika Kusini.
Nyumba zilizosombwa na mafuriko huko Ntuzuma, karibu na Durban, Afrika Kusini. AP - STR
Matangazo ya kibiashara

Hii imeelezwa kuwa dhoruba mbaya zaidi kuwahi kutokea katika taifa hilo la Afrika Kusini baada ya serikali kutangaza takwimu hizo.

Mafuriko hayo yamesababishwa na mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha  katika jimbo la KwaZulu-Natal, huku maporomoko ya udongo yakishuhidiwa pia na kuwanasa watu chini ya majengo.

Watalaam wa hali hali ya hewa wanaonya kuwa mafuriko zaidi yanatarijiwa kushuhudiwa katika siku zijazo, wakati huu shughuli za kuwaokoa watu zikitatizwa na ukungu.

Mafuriko hayo makubwa yalisabisha pia kusombwa kwa mama 12 kutoka kwenye hifadhi ya wanyamapori ya Ezemvelo KZN, lakini wamepâtikana hivi leo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.