Mazungumzo ya kitaifa ya Chad yaahirishwa hadi Februari 15
Kiongozi wa utawala wa kijeshi, Jenerali Mahamat Idriss Deby, katika ujumbe wake wa jadi kwa taifa ametangaza tarehe ya kuanza kwa mazungumzo ya kitaifa Februari 15.
Imechapishwa:
Kinyume na matarajio yote, rais wa Baraza la Mpito la Kijeshi, Jenerali Mahamat Idriss Deby, ametangaza kuwa mazungumzo ya kitaifa nchini Chad yatafanyika Februari 15.
Hata ivyo, Baraza la Mawaziri lilikuwa limepitisha kwamba mazungumzo hayo ya kisiasa yangelifanyika kati yamwezi Novemba na Desemba mwaka wa 2021.
Mazungumzo hayo, ambayo yanapaswa kuwa bila miiko, yanapaswa kuwezesha kutengenezwa kwa Katiba mpya ambayo baadaye itapitishwa kwa kura ya maoni kwa wananchi wote wa Chad. Inapaswa pia kufuata uchaguzi mkuu ulio huru, wa uwazi na wa kidemokrasia.