Pata taarifa kuu
ZAMBIA - MAZISHI

Viongozi wa Afrika wamuenzi Kenneth Kaunda

Mazishi ya kitaifa kumwaga aliyekuwa  rais wa kwanza na mwanzilishi wa taifa la Zambia, Kenneth Kaunda, aliyefariki dunia mwezi uliopita akiwa na umri wa miaka 97, yamefanyika leo jijini Lusaka.

wanajeshi wa Zambia wakiwa wameubeba mwili wa hayati Kenneth Kaunda
wanajeshi wa Zambia wakiwa wameubeba mwili wa hayati Kenneth Kaunda © afp
Matangazo ya kibiashara

Maelfu ya waoombolezaji waliwasili katika uwanja wa Mashujaa  kumwaga Kaunda, kiongozi huyo wa zamani ambaye ndiye aliyekuwa anasalia kama mmoja wa vigogo waliopigania uhuru barani Afrika.

Mwili wa Kaunda, ulibebwa na wanajeshi wa taifa hilo huku Jenereza lake likifunikwa na bendera ya nchi hiyo na kupewa heshima kwa kupigwa mizinga 21.

Viongozi mbalimbali kutoka mataifa ya Afrika wamehudhuria mazishi haya, na kumsifu Kaunda katika jitihada zake za kuhakikisha kuwa mataifa ya Afrika hasa yale yaliyo eneo la Kusini yanakuwa huru.

Uhuru Kenyatta wa Kenya ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Africa mashariki, akisemtaja kaunda Kaunda kama kiongozi aliyesimamia haki.

Mkuu wa Tume ya Umoja wa Afrika, Mouusa Faki kwa upande wake  alimkumbuka Kaunda kama, nguzo muhimu aliyeanzisha Umoja umoja wa Africa.

Kaunda, ambaye alifahamika kama KK alitawala nchi hiyo kwa miaka 27 tangu Uhuru wa nchi hiyo mwaka 1964 na atazikwa tarehe 7 mwezi Julai.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.