Pata taarifa kuu
UHISPANIA-BURKINA FASO

Madrid yathibitisha vifo vya Wahispania wawili nchini Burkina Faso

Wanahabari wawili kutoka Uhispania waliuawa baada ya kulengwa na shambulio la kushtukiza lililotekelezwa na kundi la watu wenye silaha mashariki mwa Burkina Faso dhidi ya doria inayopambana na ujangili Jumatatu wiki hii, Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez amesema.

Wanajeshi wa Burkina Faso wanafanya mazoezi ya kaskazini mwa nchi, Novemba 12, 2019 (picha ya kumbukumbu).
Wanajeshi wa Burkina Faso wanafanya mazoezi ya kaskazini mwa nchi, Novemba 12, 2019 (picha ya kumbukumbu). MICHELE CATTANI / AFP
Matangazo ya kibiashara

Raia wa Ireland pia aliuawa katika shambulio hilo, kulingana na vyanzo vitatu vya usalama nchini Burkinabe ambavyo havikutaka majina yao yatajwe. Kulingana na moja ya vyanzo hivi, mwanajeshi wa Burkina Faso pia hajulikani aliko kufuatia shambulio hili.

Serikali ya Burkina Faso imethibitisha kuwa watu wanne - ikiwa ni pamoja na raia watatu wa kigeni - walitoweka baada ya shambulio hili lakini imebainisha kuwa waathiriwa hao hawakutambuliwa rasmi kwenye picha za maiti zao zilizorushwa kwenye mitandao ya kijamii.

Waziri Mkuu wa Uhispania hata hivyo amethibitisha kwenye mtandao wa Twitter vifo vya waandishi hao wawili. "Habari mbaya kabisa imethibitishwa," ameandika Pedro Sanchez.

Ireland yashirikiana na washirika wa kimataifa kuwatambua wahusika

Wizara ya Mambo ya nje ya Ireland ilisema Jumatatu jioni kwamba ilipewa taarifa hiyo mbaya na kusisitiza kuwa inafanya kazi na "washirika wa kimataifa juu ya hali hiyo".

Kundi hilo liliripotiwa kutoweka baada ya washambuliaji wenye silaha kushambulia msafara wa vikosi vya usalama na raia wa kigeni Jumatatu asubuhi kwenye barabara inayoelekea kwenye hifadhi kubwa ya msitu wa Pama mashariki mwa nchi, serikali ya Burkina Faso imesema.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.