Pata taarifa kuu
CAR-USALAMA

Jamhuri ya Afrika ya Kati yaiweka kwenye himaya yake ngome ya waasi ya Bossangoa

Jeshi la Jamhuri ya Afrika ya Kati, likisaidiwa na washirika wake Urusi na Rwanda, wanadhibiti tena ngome ya waasi ya Bossangoa tangu Jumatano wiki hii, serikali imesema katika taarifa.

Wanajeshi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati katika eneo lililo kati ya miji ya Boali na Bangui Januari 10, 2021.
Wanajeshi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati katika eneo lililo kati ya miji ya Boali na Bangui Januari 10, 2021. AFP - FLORENT VERGNES
Matangazo ya kibiashara

Mlipuko wa machafuko yanayohusishwa na uchaguzi wa urais uliofanyika Desemba 27 umesababisha zaidi ya watu 200,000 kuyatoroka makaazi yao, hali ambayo imeendelea kusababisha bei za bidhaa mahitajio kupanda kutokana na kukosekana hali ndogo ya usalama kwa magari yanayosafirisha chakula katika maeneo mbalimbali nchini humo.

Waasi wanaosadikiwa kushirikiana na rais wa zamani François Bozizé waliudhibiti mji wa Bossangoa, mji alikozaliwa unaopatikana kilomita 260 kaskazini magharibi mwa mji mkuu Bangui, na miji mingine kadhaa baada ya Mahakama ya Katiba kutoidhinisha kuwania kwake mnamo mwezi Desemba.

Nchi hiyo, yenye utajiri wa dhahabu na almasi, na yenye wakaazi karibu milioni 5, imeshindwa kupata utulivu tangu kuzuka kwa uasi wa mwaka 2013.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.