Upinzani waapa kuendelea na maandamno Togo
Upinzani nchini Togo umesema utaendelea kuandamana kuhakikisha rais wa nchi hiyo Faure Gnansigbe anaachia ngazi. Tangu kuzuka kwa maandamno hayo watu kadhaa wamepotza maisha na wengine kujeruhiwa.
Imechapishwa:
Mwandishi wa RFI aliyeko Lome anasema ghasia kubwa zilishuhudiwa jana Jumatano katika nchi nzima kufuatia kile Upinzani unaoundwa na vyama 14 vya kisiasa ulisema kupinga mapendekezo yote yaliyotolewa na serikali ya kutaka kufanyika maridhiano ya kitaifa katika kumaliza mgogoro wa kisiasa uliopo hivi sasa.
Upinzani Umeendelea kuweka shinikizo kwa ajili ya kufanyika mazungumzo ya kisiasa na mageuzi ndani ya serikali iliyoko madarakani.
Upinzani umekua ukiandamana kwa miezi kadhaa kushinikiza kumalizika kwa uongozi wa miaka 50 wa familia ya rais wa nchi hiyo Faure Gnassingbe lakini pia wanapinga kubadilishwa kwa Katiba kwa lengo la kumsaidia rais wa sasa kuendelea kukaa madarakani.
Hata hivyo upinzani umeapa kuendelea na maandamano, huku ukishtumu polisi kutumiwa na chama tawala kwa kusababisha vifo na vurugu nchi nzima.
Upinzani umeomba vyombo vya sheria kuwafikisha mahakamani polisi waliohusika na vifo vya waandamanaji nchini humo.