Pata taarifa kuu
MAREKANI-DRC

Marekani yaamuru familia za wafanyakazi wake kuondoka DR Congo

Serikali ya Marekani inataka Familia za wafanyikazi wake wanaofanya kazi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuondoka nchini humo haraka iwezekanavyo, kwa sababu za kiusalama.

Wafuasi wa upinzani wakati wa maandamano mjini Kinshasa, Septemba 19, 2016.
Wafuasi wa upinzani wakati wa maandamano mjini Kinshasa, Septemba 19, 2016. AFP/EDUARDO SOTERAS
Matangazo ya kibiashara

Marekani inasema inahofia kuwa huenda kukatokea machafuko katika jiji kuu la Kinshasa na miji mingine, kutokana na harakati za kisiasa kama ilivyokuwa wiki iliyopita.

Hatua hii inakuja baada ya Marekani kuwawekea vikwazo washirika wawili wa rais Joseph Kabila kutokana na machafuko yaliyotokea hivi karibuni na kusababisha maafa, kumshinikiza rais wa nchi hiyo kuendelea kuwa madarakani wakati muda wake utakapofika mwisho.

Msemaji wa Serikali ya DRC Lambert Mende, ameishtumu hatua hiyo ya Marekani, na kudai inapanga kuleta machafuko nchini mwake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.