Pata taarifa kuu
SUDAN-MACHAR

Riek Machar apatishiwa matibabu Khartoum

Riek Machar, makamu wa rais wa Sudan Kusini aliyefutwa kwenye wadhifa huo hivi karibuni, yuko katika mji wa Khartoum, ambapo anapatishiwa matibabu, serikali ya Sudan imesema.

Aliye kuwa Makamu wa rais wa Sudan Kusini, Riek Machar.
Aliye kuwa Makamu wa rais wa Sudan Kusini, Riek Machar. AFP Photo:UNMISS/Isaac Alebe Avoro
Matangazo ya kibiashara

Machar yuko katika mji mkuu wa Sudan kwa ajili ya "matibabu", kulingana na taarifa iliyotolewa na serikali ya Sudan Sudan na kuchapishwa na shirika la habari la Sudan la SUNA.

"Sudan hivi karibuni ilimpokea Dk Riek Machar, kwa sababu za kiutu," serikali ya Sudan imesema.

Kwa mujibu wa serikali ya Sudan, aliyekuwa Makamu wa rais wa Sudan Kusini anahitaji "huduma za dharura za matibabu".

"Hali ya afya ya Dk Machar sasa imeimarika. Atakuwa chini ya uangalizi wa matibabu mpaka atakapoondoka kwenda katika nchi ambayo ni chaguo lake," imeongeza taarifa ya serikali.

Baada ya kufutwa kwenye wadhifa wa Makamu wa rais mwezi Julai, Riek Machar alitangazwa kukimbilia katika "nchi salama" ya ukanda wa Afrika ya Mashariki wiki iliyopita na msemaji wake, James Gatdet Diak.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.