Pata taarifa kuu
NIGERIA-INEC-UCHAGUZI-UHESABUJI-SIASA

Matokeo ya awali ya uchaguzi yatazamiwa kutangazwa Nigeria

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini Nigeria INEC, Attahiru Jega, amesema kuna uwezekano wa kumtangaza mshindi wa uchaguzi wa rais nchini humo ifikapo Jumatatu jioni kama zoezi la uhesabuji wa kura litamalizika mapema.

Mwanamama huyu, raia wa Nigeria, akipiga kura, Jumamosi Machi 28.
Mwanamama huyu, raia wa Nigeria, akipiga kura, Jumamosi Machi 28. REUTERS/Akintunde Akinleye
Matangazo ya kibiashara

Attahiru Jega amesema alitumaini jumuia ya kimataifa inaweza kupongeza namna Nigeria ilivyoendesha uchaguzi.

" Tuna amini zoezi la kupiga kura limeenda vizuri. Hatuwezi kupuuza changamoto zilizotukabili. Ni hakika haukuwa muda kamilifu lakini tunaamini kwa ujumla tumefanya vizuri, japokuwa bado tunayo nafasi ya kuzidi kuuboresha. Ndiyo maana tuliwaalika waangalizi vikiwemo vyombo vya habari na waangalizi wengine wa uchaguzi, ili kuweza kutangaza habari na tunaweza kujifunza kutokana na ripoti hizi. Tunaweza pia kuendelea kuboresha mchakato wa uchaguzi", amesema Jega.

Upigaji kura uliendelea katika siku ya pili ya uchgaguzi baada ya kutokea hitilafu katika kadi za kielektroniki na kuchelewesha usajili wa baadhi ya wapiga kura.
Matokeo ya awali yamepangwa kutangazwa saa 48 baada ya uchaguzi, na zoezi hilo litaahirishwa kufuatia namna uchaguzi ulivyofanyika kwa siku mbili mfululizo kutokana na kasoro za kiufundi, lakini uhesabuji wa kura unaendelea vizuri.

Zoezi la kuhesabu kura linashuhudiwa pia katika kitongoji cha Yaba nje kidogo ya mji wa Lagos ambapo viisanduku viliyojaa kura ziliyopigwa vilikua vikisafirishwa hadi kwenye shule moja ambayo itatumiwa kama kituo cha ukusanyaji kwa ajili ya vituo vyote vya kupigia kura katika mji kijiji cha Mainland Lagos. Maafisa wa Tume ya Uchaguzi, vikosi vya usalama laikini pia waangalizi wa mashirika mbalimbali wapo katika kituo hicho.

Tume ya uchaguzi iliahirisha uchaguzi katika maeneo kadhaa ya Nigeria kwa sababu ya hitilafu ya mitambo ya kutambua vitambulisho vya kupigia kura.

Awali msemaji wa Tume ya Uchaguzi, Kayode Idowe. amesema kuna maeneo mashine za kusoma kadi za kupigia kura hazikutumiwa kabisa kwa sababu ya hitilafu ya teknolojia.

 Rais Goodluck Jonathan pia aliathiriwa na tatizo hili na kulazimika kutimia njia ya kawaida kabla ya kupiga kura hapo mwishoni mwa juma hili.

Hata hivyo, katika maeneo ambayo zoezi hili lilikwenda vizuri kura zimeanza kuhesabiwa Jumapili mwishoni mwa juma hili.

Chama tawala PDP kimeishtumu Tume ya Uchaguzi kwa kutofanya maandalizi ya mapema kuhusu mitambo hii, huku muungano wa upinzani APC ukisisitiza umuhimu wa utumizi wa mitambo hiyo ili kuepuka wizi wa kura.

Ushindani mkubwa ni kati ya rais Goodluck Jonathan na kigogo wa upinzani Muhamdu Buhari.
Wachambuzi wa siasa nchini Nigeria wanasema huu ndio uchaguzi wenye ushindani mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika taifa hilo tangu ilipojipatia uhuru wake mwaka 1960.

Uchaguzi huu uliahirishwa kwa muda wa wiki sita ili kutoa muda kwa jeshi la serikali na yale ya nchi jirani ya  Chad, Niger na Cameroon kupambana na kundi la Boko Haram Kaskazini mwa nchi hiyo.

Rais Jonathan na mpinzani wake Buhari wameahidi kuhakikisha kuwa ghasia hazitokei nchini humo wakati wa zoezi hili na baada ya upigaji kura na watakubali matokeo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.