Pata taarifa kuu
BURKINA FASO-Katiba-Siasa

Burkina Faso: Michel Kafando ateuliwa kuwa rais wa mpito

Baada ya kucheleweshwa kwa siku moja kutokana na matatizo ya kiufundi na vifaa, mkataba wa mpito ulisainiwa siku ya Jumapili Novemba 16 katika mji mkuu wa Burkina Faso, Ouagadougou, na vikosi vya ulinzi na usalama, vyama vya siasa, viongozi wa dini pamoja na vyama vya kiraia.

Michel Kafando akiwa mstari wa mbele, mwaka 2008, wakati alikua balozi wa Burkina Faso kwenye Umoja wa mataifa.
Michel Kafando akiwa mstari wa mbele, mwaka 2008, wakati alikua balozi wa Burkina Faso kwenye Umoja wa mataifa. AFP/Issouf Sanogo
Matangazo ya kibiashara

Mapema Jumatatu Novemba 17 asubuhi, mwanadiplomasia Michel Kafando ameteuliwa kuwa rais wa mpito wa Burkina Faso.

Ni rasmi sasa, mkataba wa mpito, ambao utasaidia kuzindua shughuli za taasisi za mpito, ulisainiwa kwa vifijo na nderemo na wadau wote waliochangia kwa kupatikana suluhu katika mgogoro uliyokua ukiendelea nchini Burkina Faso.

Watu kutoka makundi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama,vyama vya siasa, vyama vya kiraia, viongozi wa kidini na kimila.

Vifijo na nderemo vilisikika wakati Luteni Kanali Zida alipoinua mikono yake iliyokua ikishikilia nakala ya mkataba huo uliyosaniwa. Kiongozi wa upinzani, Zephyrinus Diabré, Amadou Dabo, mbunge wa zamani wa chama tawala cha Blaise Compaoré, mwanasheria Luc Marius Ibriga ambae amekua akiwakilisha vyama vya kiraia pamoja na padri Henri Yé, aliye wakilisha dini wamepongeza hatua hiyo.

Wadau katika mgogoro uliyokua ukiendelea Burkina Faso wakitia saini katika mkataba wa mpito unaopelekea kuundwa kwa taasisi za mpito za uongozi wa nchi, Ouagadougou, Novemba 16 mwaka 2014.
Wadau katika mgogoro uliyokua ukiendelea Burkina Faso wakitia saini katika mkataba wa mpito unaopelekea kuundwa kwa taasisi za mpito za uongozi wa nchi, Ouagadougou, Novemba 16 mwaka 2014. RFI/Guillaume Thibault

Michel Kafando, mwenye umri wa miaka 72 aliwahi kuwa balozi wa Haute-Volta katika miaka ya 1980, na baadae balozi wa Burkina Faso kati ya miaka 1998 na 2011. Wagombea wengine wawili waliokua katika kinyanganiro hicho ni Joséphine Ouedraogo, waziri wa zamani katika utawala wa thomas Sankara, pamoja na mwandishi wa habari Cherif Sy.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.