Rais wa Nigeria apuuza matakwa ya Boko Haram
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amekataa pendekezo la kundi la kigaidi la boko Haram kuwaachilia wanamgambo wake wanaozuiliwa ili kundi hilo liwaachilie huru wasichana zaidi ya 200 waliotekwa nyara mwezi mmoja uliopita.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Waziri wa Uingereza anayehusika na maswala ya Afrika Mark Simmonds amewaambia waandishi wa habari jijini Abuja kuwa walizungumzia suala hilo na rais Jonathan akakataa kushauriana na kundi hilo kuhusu kuachiliwa kwa wafungwa hao.
Hata hivyo, waziri huyo wa Uingereza amesisitiza kuwa serikali ya Nigeria iko tayari kuzungumza na kundi hilo ili kuachiliwa huru wasichana hao na kutokomeza vitendo hivyo vya ugaidi nchini humo.
Kiongozi wa kundi la Boko Haram, abubakar Shekau, alipendekeza fikra hio ya kubadilichana wasichana waliyotekwa nyara na wanamgambo wa kundi lake wanaozuiliwa katika mkanda wa video uliyorushwa hewani jumatatu, huku ukiwaonyesha wasichana hao waliyotekwa nyara katika shule la Chibok, linalopatikana katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Mapema juzi jumanne, waziri wa mambo ya ndani Abba Morro alipinga pendekezo hilo, huku akikatalia kundi la Boko Haram kutoa mashari, iwapo itataka mazungumzo na serikali.
Wakati huo huo juzi jumanne waziri wa masuala maalum, Taminu Turaki, alisema serikali ya Nigeria iko tayari kuketi pamoja na kundi la Boko Haram ili mradi tu wasichana waliyotekwa nyara waachiliwe.
Kwa sasa Marekani inaongoza operesheni maalum wakitumia ndege maalum kuwatafuta wasichana hao ambao hawajulikani walipo.