Pata taarifa kuu
ALGERIA-Usalama

Kundi la Aqmi lakiri kuwaua wanajeshi 11 nchini Algeria

Kundi la wanamgambo wa kislamu lenye mafungamano na kundi la Al Qaeda Aqmi, limekiri kutekeleza aprili 19 shambulio dhidi ya msafara wa magari ya jeshi. Kundi hilo limethibitisha shambulio hilo katika tangazo ambalo limetoa leo. Kwa mujibu wa takwimu rasmi ziliyotolewa, shambulio hilo liligharimu maisha ya wanajeshi 11. 

Droukdel, akijulikana kwa jina la Abou Moussa Abdelouadoud, raia wa Algeria,ambaye ni mmoja wa viongozi wa kundi la Aqmi.
Droukdel, akijulikana kwa jina la Abou Moussa Abdelouadoud, raia wa Algeria,ambaye ni mmoja wa viongozi wa kundi la Aqmi. AFP PHOTO/HO
Matangazo ya kibiashara

Usiku wa tarehe 19 aprili, wanamgambo wa kundi hilo la Aqmi lenye mafungamano na kundi la Al Qaeda lilitekeleza shambulio la kuvizia dhidi ya msafara wa magari ya jeshi katika eneo la boudrarène katika mji wa Kabylie, mashariki mwa mji wa Alger.

Tangazo hilo limefahamisha kwamba wanajeshi zaidi ya thelathini ndio waliyouawa katika shambulio hilo na wengine wengi walijeruhiwa , huku kundi hilo la Aqmi likibaini kwamba lilipoteza mpiganaji wake mmoja.

Kundi la wanamgambo wa kislamu wenye mafungamano na kundi la A Qaeda (Aqmi) lina ngome katika maeneo ya mipaka ya Algéria, Niger, Mali na Mauritani , kama inavyoonyesha ramani hii.
Kundi la wanamgambo wa kislamu wenye mafungamano na kundi la A Qaeda (Aqmi) lina ngome katika maeneo ya mipaka ya Algéria, Niger, Mali na Mauritani , kama inavyoonyesha ramani hii. RFI/Latifa Mouaoued

Shambulio hilo liliotekelezwa baada ya uchaguzi mkuu wa urais uliyofanyika aprili 17 dhidi ya wanajeshi waliokua wakilinda usalama wa uchaguzi,ulisababisha hali ya taharuki katika taifa la Algeria, ambalo katika miaka ya 1990 lilikumbwa na machafuko ya wenyewe kwa wenyewe.

Jeshi la Algeria bado linakabiliana na mashambulizi ya wanamgambo wa kundi la Aqmi.
Jeshi la Algeria bado linakabiliana na mashambulizi ya wanamgambo wa kundi la Aqmi. AFP PHOTO / FAROUK BATICHE

Kwa mujibu wa takwimu rasmi ziliyotolewa baada ya shambulio hilo, wanajeshi 11 waliuawa na wengine watanu walijeruhiwa vikali, huku waasi watatu wakiwa waliuawa.

Aqmi, kwa upande wake imehakikisha kwamba mmoja miongoni mwa wapiganaji wake , ambaye anajulikana kwa jina la Abu Anas, mkaazi wa Monstaganem (kaskazini magharibi mwa Algeria).

Wapiganaji wa kundi la Al-Tawhid Wal Jihad wanaojulikana kwa jina la “Simba” walijilipiza kisase “kwa ndugu yao aliyeuawa kikatili”, limemalizia tangazo hilo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.