Polisi ya Tanzania yakana 'kumteka' mwanahabari Erick Kabendera
Polisi ya Tanzania imekana kumteka mwanahabari Erick Kabendera na kuainisha kwamba mwandishi huyo wa habari anashikiliwa na vyombo vya usalama na anahojiwa kuhusu uhalali wa uraia wake.
Imechapishwa:
Kamanda Wa Kanda Maalumu Lazaro Mambosasa anasema Polisi ilimpa wito Wa kumwita kwa Mahojiano lakini Hakufika.
"Huyu mtu hajatekwa, anashikiliwa na yupo kituoni Hapa, tunachunguza Uraia wake kwa kushirikiana na uhamiaji,"
Hata Hivyo Mambosasa hajaeleza kwa kina kwa nini jeshi hilo linachunguza uraia Wa Mwanahabari huyo na Kusema akisema huenda akaharibu uchunguzi.
Amewataka Watanzania kuepuka Habari zinazoweza kuzua taharuki.
Erick Kabendera amewahi kuandikia magazeti kadhaa ya ndani na nje ya Tanzania na ni mmoja wa wanahabari wanaoheshimika kwa kazi zao.