Katumbi: Rais Kabila bado hajajibu maswali ya msingi
Mgombea urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi, amesema nchi yake inaelekea pabaya kwa vile Rais Joseph Kabila hajajibu masuala ya msingi yanayofukuta kisiasa nchini humo.
Imechapishwa:
Kiongozi huyo wa upinzani ambaye yuko nje ya nchi kwa sababu za kiafya amesema kuwa, dhamira ya rais kabila ya kuendelea kutojibu baadhi ya masuala yenye utata ni hali itakayiongiza nchi hiyo katika "mgogoro mbaya zaidi ".
Aidha, Katumbi amesema, Rais Kabila hajatumia fursa ya maadhimisho ya uhuru kuwahakikishia wananchi kuhusu nia ya kuondoka madarakani tarehe 19 Desemba na kuitishwa kwa uchaguzi tarehe 20 septemba mwaka huu kulingana na katiba ya Congo.
Chers amis, voici ma déclaration en ce jour de l'indépendance en #RDC. Très bonne fête à tous mes compatriotes! pic.twitter.com/5C2MPkNDNg
— Moise Katumbi (@moise_katumbi) June 30, 2016
Mbali na hayo, Katumbi ambaye hivi karibuni alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela katika kesi ya ulaghai, amesema kuwa huo ni "upotoshaji kamili ili kumzuia mgombea urais na kwamba huo ni unyanyasaji ambao hautathiri uamuzi wake.
Siku mbili kabla ya uhuru wa Congo, Rais Kabila Kabange akiwa mjini Kalemie, katika ujumbe wake kwa taifa, alielezea dhamira yake ya kuandaa uchaguzi nchini Congo lakini bila ya kubainisha ni lini uchaguzi huo utafanyika.