Pata taarifa kuu
KENYA-NDOA

Harusi za usiku zapigwa marufuku Mombasa

Sasa ni ni marufuku kuandaa sherehe za harusi usiku katika mji wa Mombasa, kusini mwa Kenya. Mkuu wa polisi katika kaunti ya Mombasa, Maalim Mohammed ameeleza kwamba hatua hii ina lengo la kuimarisha usalama katika eneo hilo.

Askari polisi apiga doria katika mji wa Mombasa, lNovemba 17, 2014.
Askari polisi apiga doria katika mji wa Mombasa, lNovemba 17, 2014. AFP PHOTO/IVAN LIEMAN
Matangazo ya kibiashara

Kwa hauta hii wakazi wa mji watalindwa kutokana na mashambulizi ya visu na yanayoendeshwa na magenge ya watu.

Hivi karibuni, makundi ya uhalifu yameongezeka mjini Mombasa.

Katika baadhi ya vitongoji, watu wana wamearifu kuwa vitendo vya ujambazi vimekua vikifanyika mchana kweupe.

Wahalifu wengi kutoka makundi hayo tayari wamekamatwa na polisi ambayo inaendelea na shughuli hizokatika maeneo mbalimbali.

Kwa ujumla, sherehe za harusi zinadumu hadi siku tano mjini Mombasa, pamoja na sikukuu siku nzima na usiku.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.