Miili 39 yapatikana katika lori Essex, Uingereza
Miili thelathini na tisa imepatikana katika lori usiku wa Jumanne kuamkia Jumatano wiki hii katika eneo la Grey, jijini Essex, mashariki mwa London.
Imechapishwa:
Dereva, mwenye umri wa miaka 25, mwenye asili ya Ireland Kaskazini, amekamatwa kwa mauaji, polisi ya Uingereza imetangaza. Kulingana na ripoti ya awali ya uchunguzi, lori hilo lilitoka Bulgaria na liliingia Uingereza Jumamosi, Oktoba 19 likipitia Holyhead, bandari inayopatikana kwenye pwani ya magharibi mwa Uingereza.
Hakuna maelezo yaliyotolewa kuhusu nchi wanakotoka waathiriwa. haijulikani ikiwa wathiriwa walikuwa wahamiaji.
"Mchakato wa kutambua miili unaendelea," mkuu wa polisi wa mji wa Essex, Andrew Mariner, amesema katika taarifa.
Wahamiaji wengi wamekuwa wakijaribu kuingia Uingereza katika miaka ya hivi karibuni kwa kujificha katika kasha za gari za mizigo au katika boti. Polisi imezingira eneo Waterglade ambapo gari hilo limeegeshwa na watu wamepigwa marufu kukaribia eneo hilo.
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema, "ameshtushwa" na habari hii. Ameendelea kusema, "Ninaungana kwa huzuni na familia zilizopoteza wapendwa wao. "
I’m appalled by this tragic incident in Essex. I am receiving regular updates and the Home Office will work closely with Essex Police as we establish exactly what has happened. My thoughts are with all those who lost their lives & their loved ones.
Boris Johnson (@BorisJohnson) October 23, 2019