Pata taarifa kuu
UINGEREZA-EU-USHIRIKIANO

Mkataba mpya wa Brexit wafikiwa kati ya Uingereza na Umoja wa Ulaya

Mkataba mpya wa Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya umefikiwa Alhamisi wiki hii, Oktoba 17, kabla ya mkutano muhimu wa Umoja wa Ulaya.

Michel Barnier, kiongozi mkuu katika mazunguymzo ya Umoja wa Ulaya na Uingereza kuhusu Brexit, amekaribisha mkataba wenye "haki na wenye busara" kuhusu Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya.
Michel Barnier, kiongozi mkuu katika mazunguymzo ya Umoja wa Ulaya na Uingereza kuhusu Brexit, amekaribisha mkataba wenye "haki na wenye busara" kuhusu Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya. REUTERS/Francois Lenoir
Matangazo ya kibiashara

Rais wa Tume ya Ulaya Jean-Claude Juncker ametangaza kwenye Twitter kuwa mkataba umefikiwa mjini Brussels. Boris Johnson pia ameandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter akikaribisha "mkataba mpya mzuri".

Mkataba huu ambao umefikiwa baada ya mazungumzo ya muda mrefu ambayo yametajwa na Jean-Claude Juncker kama "ya haki na usawa" yanaweza kuanza kutumika Novemba 1, 2019.

Nakala hii sasa itawasilishwa kwa Wakuu wa Nchi na Serikali ambao walikuwa wanatarajiwa kufanya kikao chao cha kwanza cha kazi jijini Brussels baadaye leo alaasiri.

Viongozi hao wanatarajia kutoa idhni yao kwa mapendekezo ya Michel Barnier, ambaye amesema watu wasisubiri maajabu, kwa hatua hii.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.