UINGEREZA-EU-USHIRIKIANO
Theresa May ajikuta kwenye wakati wakati mgumu
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May, amekuwa katika harakati za lala salama, kuwashawishi wabunge kuunga mkono mkataba uliofikiwa kati ya nchi hiyo na Umoja wa Ulaya, kuhusu namna nchi hiyo itakavyokuwa baada ya kujiondoa kwenye umoja huo mwezi Machi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wabunge wanatarajiwa kupigia kura mswada huo siku ya Jumanne wiki hii huku kukiwa na wasiwasi kuwa huenda wakaukataa.
May amesema iwapo, wabunge wataukataa mkataba huo, itamaanisha kuwa wanataka nchi hiyo isalia kwenye Umoja wa Ulaya.
Viongozi wa Umoja wa Ulaya, wamesema hawewezi kuja tena katika meza ya mazungmzo kujadili upya mkataba huo.