Pata taarifa kuu
UINGEREZA-EU-MAY

Uingereza yataka heshima kutoka kwa viongozi wa Umoja wa Ulaya

Waziri Mkuu wa Uingereza Teresia May ameitaka Umoja wa Ulaya, kuiheshimu nchi yake wakati huu majadiliano yakiendelea kuhusu namana nchi hiyo  itakavyojiondoa kwenye Umoja huo.

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May Jack Taylor/Pool via Reuters
Matangazo ya kibiashara

May amesema viongozi wa Umoja huo kukataa mpango wake wa namna Uingereza itakavyojiondoa katika Umoja huo, kuhusu masuala ya biashara, ajira na mipaka  ni suala ambalo halikubaliki.

Uigereza inatarajiwa kujiondoa kabisa katika Umoja huo kufikia tarehe 29 mwezi Machi mwaka ujao kwa mujibu wa mkataba uliounda Umoja huo.

Rais wa Baraza hilo Donald Tusk amesema yupo tayari kuendelea kuzungumza na Uingereza na badala yake kusema Waziri Mkuu May ndiye anayeonesha ugumu katika mazungumzo haya.

Uingereza imetishia kujiondoa katika mazungumzo hayo iwapo haitasikilizwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.