Ufaransa yaishtumu Italia kukataa kuwapokea wahamiaji
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameishutumu Serikali ya Italia kwa kutowajibika baada ya nchi hiyo kukataa kuwapokea wahamiaji na kuwaacha kwenye sintofahamu katika meli iliyokuwa imewaokoa kwenye bahari ya Mediterania.
Imechapishwa:
Meli ya Aquarius ambayo imebeba wahamiaji 629 itasindikizwa na meli nyingine mbili za jeshi la wanamaji wa Italia kuwapelekea wahamiaji hao nchini Uhispania kwenye mji wa Valencia ambako Serikali imekubali kuwapokea.
Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Ufaransa, Jean-Yves Le Drian ametupilia mbali madai kuwa nchi yake imekuwa ikikwepa kuwapokea wahamiaji na kuiachia Italia peke yake.
Haya yanajiri wakati huu maelfu ya wahamiaji wakiendelea kufanya safari za hatari kupitia bahari ya mediterania kuingia barani Ulaya kutafuta maisha na nchi ya Italia imekuwa kituo chao kikuu.