Serikali ya Uhispania yakutana kwa dharura
Siku moja baada ya hotuba ya Carles Puigdemont kutangaza kusitisha mchakato wa uhuru katika jimbo lake, serikali kuu ya Uhispania inakutana ili kujadili hali inayoendelea katika jimbo hilo.
Imechapishwa:
Mkutano huo wa dharura unafanyika Jumatano hii, wakati ambapo rais wa Catalonia alisaini hati ya kujitenga kwa jimbo la Catalonia, licha ya kusita kutangaza uhuru wa jimbo hilo, akisema kuna haja ya kufanya mazungumzo katika ngazi ya kitaifa na ile ya kimataifa kuhusu uhuru a Catalonia.
Kikao cha Baraza la Mawaziri, chini ya uenyekiti wa Mariano Rajoy, Waziri Mkuuu wa Uhispania kimepangwa kufanyika saa 9 asubuhi saa za Uhispania, kuamua hatua za kuchukua siku moja baada ya kikao cha ubunge cha bunge Catalonia.
Kutokana na shinikizo kutoka pande zote, pamoja na Ulaya, rais wa jimbo la Catalonia, Carles Puigdemont, aliahidi kubadilisha Catalonia kuwa "Jamhuri" huru, huku akiomba kusitishwa kwa mchakato huo kwa kusubiri kupata "ufumbuzi" kutoka katika mazungumzo na serikali kuu ya Madrid.