Pata taarifa kuu
UTURUKI-EU-USHIRIKIANO

Erdogan: Umoja wa Ulaya unatupotezea muda

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameliambia Shirika la Habari la Uigereza BBC kuwa nchi yake haitaona tatizo ikiwa ombi la nchi yake kuungana na Umoja wa Ulaya litakataliwa.

Turkish President Recep Tayyip Erdogan gives a press conference after the G20 summit in Hamburg, Germany
Turkish President Recep Tayyip Erdogan gives a press conference after the G20 summit in Hamburg, Germany Reuters/Wolfgang Rattay
Matangazo ya kibiashara

Aidha rais Erdogan amesema nchi yake inaweza kusimama peke yake na kuongeza kuwa umoja huo unaipotezea nchi yake muda.

Kiongozi huyo pia amepinga madai kuwa serikali yake imewafunga jela wanahabari 150.

Hivi karibuni Uturuki ilikumbwa na hali ya sintofahamu, siku chache tu baada ya kushundwa kwa jaribio la mapinduzi. Baada ta kisa hicho, serikali ya Erdogan iliwafunga maafisa mbalimbali wa jeshi na polisi bila kusahau maafisa wengine serikalini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.