MAKEDONIA-USALAMA
Waandamanaji washambulia majengo ya Bunge Makedonia
Waandamanaji wamevamia majengo ya bunge nchini Makedonia baada ya kuchaguliwa kwa Spika kutoka kwenye kabila la Albania. Hali ya machafuko imeendelea kushuhudiwa nchini humo kufuatia maandamano yanayoendelea.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Makabiliano yalizuka na kusababisha majeruhi ya watu 10 wengi wakionekana kutokwa na damu.
Kiongozi wa chama kilicho na wabunge wengi Zoran Zaev, pia alijikuta katika vurugu hizo na kujeruhiwa vibaya.
Kumekuwa na maandamano ya wiki kadhaa kushinikiza kuitishwa kwa uchaguzi mpya.