Pata taarifa kuu
UFARANSA-SIASA

Kampeni za urais nchini Ufaransa zaingia kipindi cha lala salama

Ni wiki moja kamili kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi wa urais nchini Ufaransa tarehe 23 mwezi huu wa Aprili. 

François Fillon mgombea wa urais nchini Ufaransa
François Fillon mgombea wa urais nchini Ufaransa REUTERS/Jean-Paul Pelissier
Matangazo ya kibiashara

Kampeni zimeingia katika dakika za lala salama, huku wagombea wakisalia na siku chache kunadi sera zao mbele ya rais wa Ufaransa ambao Jumapili ijayo watapiga kura, kuamua ni nani atakuwa rais wao.

Uchaguzi wa Jumapili ijayo, utakuwa ni wa awamu ya kwanza. Mshindi anahitaji kupata thuluthi mbili ya kura zote ili kutangazwa mshindi.

Hata hivyo, inavyoonekana kutakuwa na duru ya pili ya Uchaguzi huo tarehe 7 mwezi Machi.

Rais wa sasa Francois Hollande hawatania tena, uamuzi ambao aliufanya mwezi Desemba mwaka uliopita.

Kati ya wagombea 11 wanaotafuta urais, wachambuzi wa siasa wanaona  kuwa ushindani mkali utakuwa kati ya Marine Le Pen, Emmanuel Macron, Francois Fillion na Benoit Hammon.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.