Scotland kubaki EU, aonya Alex Salmond
Wanasiasa wengi nchini Scotland hawapendelei kuona nchi yao inajiondoa katika Umoja wa Ulaya, wakibaini kwamba ni moja ya njia muhimu wa kudumisha umoja na maendelea katika nchi wanachama wa umoja huo.
Imechapishwa:
Alex Salmond, kiongozi wa zamani wa chama cha mrengo wa kushoto cha SNP na Waziri Mkuu wa zamani (2007-2014), amesema anaunga mkono nchi yake kubaki katika Umoja wa Ulaya.
Mbunge katika Bunge la Westminster, msemaji wa kundi la Wabunge kutoka chama cha SNP kwa masuala ya Mambo ya Nje, Alex Salmond, mwenye umri wa miaka 61, amekua akiendesha kampeni kama chake kwa ajili ya kubaki katika Umoja wa Ulaya. Scotland ilifuata nasaha hiyo ya Bw Salmond ya kupiga kura 62% dhidi ya kujiondoa katika Umoja wa Ulaya.
Akihojiwa swali kuhusu kura pili ya maoni juu ya uhuru nchini Scotland?, Alex Salmond, amejibu akisema: "Nicola Sturgeon (Waziri Mkuu wa sasa wa Scotland) anajaribu kufanya kilio chini ya uwezo wake kwa kulinda maslahi ya Scotland. Lengo la mazungumzo ya sasa ni kuhakikisha kuwa Scotland haijiondoi katika Umoja wa Ulaya."