VATICAN-PAPA-JAMII
Papa Francis awateua Makadinali wapya
Kiongozi wa Kanisa duniani Papa Francis amewateua Makadinali 20 wapya wengi wao kutoka bara la Afrika, Asia na Latin America.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Makadinali 15 kati ya ishirini walioteuliwa wana umri wa chini ya miaka themanini na hivyo wanaingia katika kundi la Makadinali walio na jukumu la kumchagua kiongozi mpya wa kanisa hilo.
Askofu Soane Patita Paini Mafi kutoka Tonga mwenye umri wa miaka 53 anakuwa Kadinali mwenye umri mdogo kuwahi kuteuliwa katika wadhifa huo.
Msemaji wa Vatican Father Federico Lombardi amesema hakuna Makadinali walioteuliwa kutoka Marekani na Canada kwa sababu nchi hizo zina Makadinali wa kutosha.