Mwanamuziki Prince amefariki akiwa na umri wa miaka 57
Tovuti ya Marekani ya TMZ imetangaza Alhamisi hii, Aprili 21, kifo cha mwanamuziki Prince. Taarifa hii imethibitishwa na afisa wa mawasiliano ya nyota huyo.
Imechapishwa: Imehaririwa:
I can’t believe it, I’m in total shock. So many wonderful memories,
— Lionel Richie (@LionelRichie) April 21, 2016
I will miss him. #Prince
"Today, the world lost a creative icon." —@POTUS on the passing of @Prince: https://t.co/MTb3nKxruR pic.twitter.com/gowq1MExM3
— The White House (@WhiteHouse) April 21, 2016
And just like that...the world lost a lot of magic ✨ Rest in peace Prince! Thanks for giving us so much...
— KATY PERRY (@katyperry) April 21, 2016
RIP Prince. So sad. pic.twitter.com/um8Dqy3pDL
— Lori Mayfield (@lorilei1) April 21, 2016
For you #PRINCE .I will always love you. Rest in Purple Rain https://t.co/Qj0hIF0WxK
— Kasia Nova (@KASIA_NOVA) April 21, 2016
Prince ambaye alikua akijulikana kwa jina la utani la "The Artis" alifuta tamasha mbili kutokana na matatizo ya kiafya. Mashabiki wake watakumbuka hasa albamu yake ya "1999", iliyomfikisha katika jukwaa la kimataifa.
Prince ambaye alipata umaarufu kwa nyimbo zake kama vile Purple Rain na Kiss alikutwa amekufa katika studio zake za Paisley Park, katika jimbo la Minnesota,tovuti ya TMZ imearifu. Mwanamuziki mashuhuri wa mtindo wa Funk alilazwa hospitalini Ijumaa Aprili 15 kufuatia dalili zinazohusiana na mafua.
"Ni kwa huzuni mkubwa ninathibitisha kwamba mwimbaji mashuhurii, Prince Roger Nelson, amefariki nyumbani katika mji wa Paisley Park asubuhi hii," msemaji wake, Yvette Noel-Schure, amebaini.
Fikra
Prince Roger Nelson alizaliwa mwaka 1958 katika mji wa Minneapolis, na kupewa jina la utani la "mtoto kutoka Minneapolis". Alikuwa mwembambana alikua akipima mita 1.60 za urefu, lakini alikuwa alikua mwanamuziki mashuhuri, mwenye uwezo wa kushawishi pande zote, na kutunga au kuimba nyimbo zote za watu weusi : jazz, funk, hip-hop, soul.